Cardi B Adai Offset Hamsaidii Kulea Watoto

Cardi B Adai Offset Hamsaidii Kulea Watoto

Baada ya kusubiliwa kwa muda mrefu jina la mtoto wa tatu wa rapa Card B aliyezaa na aliyekuwa mpenzi wake mwanamuziki Offset, na sasa Cardi amefuchua jina la mtoto huyo aitwaye Blosson aliyezaliwa Septemba 2024.

Cardi alifichua jina hilo siku ya jana, Mei 30, akiwa kwenye X Spaces ambapo wakati huohuo alimshutumu Ex wake Offset, kwa kutotumia muda wake mwingi na mtoto wao aliyezaliwa.

Amesema kuwa hajawahi kumzuia Offset kuwaona watoto wao lakini amemuona Blosson mara tano tu tangu azaliwe.

“Kiari anaruhusiwa kuwaona watoto wangu. Hakuna siku hata moja ambayo haruhusiwi kuwaona watoto wangu. Alisimama watoto wangu mara tatu. Amemwona Blossom kama mara tano tu" amesema Card B.

Card B amesema licha ya Offset kuzungumza na wanawe kila siku lakini bado anahitaji kuona binti yake anapata upendo wa baba.

“Unazungumza na watoto karibu kila siku moja. Ninakuruhusu kuzungumza na watoto kila siku. Nikikuruhusu kuzungumza na watoto, kwa nini nisikuruhusu kuwaona watoto? Nataka binti yangu ahisi upendo wa baba yake." amesema Card B.

Cardi pia alidai kuwa mara ya mwisho Offset kutumia muda wake na watoto ilikuwa mwezi Machi 2025.

Offset na Cardi kwa sasa wametalakiana Cardi anadai kwamba alivunjika moyo baada ya Offset kuomba usaidizi wa mume na mke kwenye malezi ya watoto wao baada ya ndoa yao kuvunjika.

Wawili hao wamebarikiwa watoto watatu ambao ni Kulture (6), Wave (3), na Blosson aliyezaliwa Septemba 7, 2024, Wanandoa hao wa zamani walionekana wakiwa wameketi na watoto wote katika picha ya pamoja kwenye chumba cha hospitali muda mchache baada ya Blosson kuzaliwa.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Masoud Kofii


Latest Post

Latest Tags