Benki ya Dunia: Umaskini uliokithiri utaendelea kuwepo

Benki ya Dunia: Umaskini uliokithiri utaendelea kuwepo

Hellow! Watu wangu wa nguvu, kama kawaida yetu tunazidi kukujuza kuhusiana na habari mbalimbali. Basi bwana Benki ya Dunia imesema sio rahisi ulimwengu kulifikia lengo lake la kuondoa umaskini uliokithiri ifikapo mwaka 2030. Hayo yameelezwa katika ripoti mpya ya Benki ya Dunia iliyotolewa hapo jana.

Ripoti hiyo iliyopewa jina ''Umaskini na Ustawi wa Pamoja'' inaelezea maendeleo katika juhudi za kimataifa za kumaliza umaskini uliokithiri. Ripoti hiyo imelitaja janga la virusi vya corona kama kizuizi kikubwa katika juhudi za kupunguza umaskini duniani kwa miongo kadhaa.

Kwa mujibu wa Benki ya Dunia, mwaka 2020 ulishuhudia zaidi ya watu milioni 71 wakiishi kwa dola 2.15 kwa siku au chini ya hapo.

Aidha wachumi wa benki hiyo wamesema hali imekuwa mbaya zaidi baada ya Urusi kuivamia Ukraine pamoja na kusuasua kwa uchumi wa China, mfumuko wa bei na kuongezeka kwa bei ya chakula na nishati. Hatua hizo zinaendelea kukwamisha maendeleo katika siku zijazo.

Chanzo DW






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post