Baba mzazi wa kocha Nabi afariki dunia

Baba mzazi wa kocha Nabi afariki dunia

Aliyekuwa ‘Kocha’ Mkuu wa ‘Klabu’ ya Yanga Nasreddine Nabi amefiwa na baba yake mzazi asubuhi ya leo.

Taarifa ya kifo chake imetolewa na aliyekuwa Msemaji wa ‘Klabu’ hiyo Haji Manara kupitia ukurasa wake wa Instagram kwa kueleza kuwa amepokea taarifa dakika chache zilizopita kuwa ‘Kocha’ wa zamani wa ‘klabu’ hiyo amefiwa na baba yake mzazi asubuhi ya leo huko Monastir nchini Tunisia.

Aidha aliendelea kwa kueleza kuwa amepata wasaa wa kuongea na Nabi mchana huu na kuthibitisha taarifa hizo ili kuwajulisha watanzania na mashabiki ambao walikaa na kocha Nabi vizuri.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post