Baba Levo: Mungu baba kama ni kosa kumshabikia Diamond nitoe roho

Baba Levo: Mungu baba kama ni kosa kumshabikia Diamond nitoe roho

Mwanamuziki na mtangazaji #BabaLevo ammwagia sifa #DiamondPlatnumz Kupitia ukurasa wake wa Instagram ame-share video ya nyota huyo wakati anatumbuiza na kuandika ujimbe akisema kama kweli kumshabikia Diamond ni kosa basi Mungu aitoe roho yake.

Baada ya Diamond kuonesha tena ubunifu wake wa kuingia kama mjapani kwenye tamasha lilofanyika jana usiku Sumbawanga.

Baba Levo ameandika “Eeeh Mungu baba kama kweli kumshabikia Diamondplatnumz #Lukuga, #SamHo'ng ni Kosa, basi itoe roho yangu hapa dubaii. kaipandisha china jukwaani, ila kama sio kosa acha wenye chuki waende mahakamani".
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post