Baba Levo ampa Alikiba maua yake

Baba Levo ampa Alikiba maua yake

Baada ya mkali wa sauti #Alikiba kutoa ngoma ya Amapiano inayoenda kwa jina ka #Sumu aliyo mshirikisha #Marioo, Chawa wa Taifa Baba Levo, ameonekana kuvutiwa na ngoma hiyo na kumtaka #AliKiba aendelee na muziki huo na azidi ku-promote nyimbo zake kwa vibe kali.

Licha ya #AliKiba kuwahi kutoa kauli ya kutofanya muziki wa #Amapiano na  kuwaachia wasanii wengine wakizidi kupata fan base kupitia muziki huo, ngoma yake ya #Sumu imeonesha kupendwa mashabiki zake.

Kwenye moja #Interview aliyofanya #BabaLevo alijikuta akimpa #AliKiba maua yake kwa kusema “alikiba sasahivi ndio ameanza kupromote ngoma, yani halali anafanya kazi usiku na mchana

 Ile kauli yake alisema hata imba amapiano sasahivi ataimba hadi singeli kwasababu usipoendana na biashara iliopo unapotea kimuziki mtu yeyote anaye pinga amapiano hajui biashara muziki unapenda mambo hayo maana bila kelele hutoboi”






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post