Antony afutiwa mashitaka ya unyanyasaji na Ex wake

Antony afutiwa mashitaka ya unyanyasaji na Ex wake

Mchezaji wa ‘klabu’ ya #ManchesterUnited, Antony Dos Santos aliyefunguliwa mashtaka na wanawake watatu kuhusu unyanyasaji na kuwashambulia, inadaiwa mmoja kati ya hao wanawake amefuta mashtaka yake dhidi ya nyota huyo wa Brazil.

Winga huyo mwenye umri wa miaka 23 kwa sasa yupo nje ya majukumu ya ‘Klabu’ yake kwa ajili ya kushughulikia tuhuma hizo ikiwemo kutoka kwa aliyekuwa mpenzi wake, #GabrielaCavallin ambapo upelelezi unafanywa na Polisi wa #Brazil na #England.

Aliyefuta mashtaka ni mwanamke aliyefahamika kwa jina la Ingrid Lana aliyedai alifanyiwa unyanyasaji Oktoba 2022.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post