Amaju amtaka Davido aombe msamaha siku nne mfululizo

Amaju amtaka Davido aombe msamaha siku nne mfululizo

Waandaaji wa tamasha la ‘Warri Again Concert’ wamemfungulia kesi ya madai ya N2.3 bilioni msanii kutoka nchini Nigeria Davido kwa madai ya kukiuka makubaliano ya kimkataba waliyoingia kati yao.

Tamasha hilo linalofanyika kila mwaka linalomilikiwa na aliyekuwa Rais wa Shirikisho la Soka nchini humo Amaju Pinnick, aliwasilisha kesi mbele ya mahakama kuu ya jimbo la Delta, huku mshitaki huyo akitaka Davido na 'lebo' yake kutoa fidia ya N2 bilioni.

Mshitaki huyo aliiomba mahakama kumtaka Davido kugharamia pesa ya mwanasheria na gharama za kufungua kesi pia anataka mahakama hiyo imuamuru mwanamuziki huyo kuomba msamaha kwenye mitandao yake yote ya kijamii na kwenye magazeti mawili yanayotoka kila siku kwa siku nne mfululizo.

Hii inakuja baada ya Davido kushindwa kufuata mkataba waliosaini na Amaju kuhusiana na tamasha hilo.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post