Aliyetunga wimbo wa Sarafina afariki

Aliyetunga wimbo wa Sarafina afariki

Mwanamuziki kutoka nchini Afrika Kusini Mbongeni Ngema, ambaye ndiye muandishi wa wimbo wa ‘Sarafina’ amefariki katika ajali ya gari Jumatano jioni akiwa na umri wa miaka 68 iliyotokea kwenye jimbo la Eastern Cape.

Taarifa hiyo ilitolewa na familia yake ikieleza kuwa Ngema aliaga dunia baada ya gari alilokuwa amepanda kugongana na jingine, alipokuwa akirejea kutoka msibani.

Mbongeni Ngema alitambulika zaidi baada ya kutunga wimbo maarufu wa ‘Sarafina’ uliokuwa ukielezea ghasia za wanafunzi katika kipindi cha ubaguzi wa rangi Soweto.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post