Aliyekuwa akishikiria rekodi ya kuwa mzee zaidi afariki dunia

Aliyekuwa akishikiria rekodi ya kuwa mzee zaidi afariki dunia

Mwanaume mmoja aitwaye Juan Vicente Perez Mora, kutoka nchini Venezuela ambaye pia alikuwa akishirikiria rekodi ya kuwa mwanamume mzee zaidi duniani amefariki dunia akiwa na miaka 114.

Taarifa ya kifo chake ilitolewa na ‘Guinness World Records’ siku ya jana kupitia mitandano yao ya kijamii, mzee huyo aliingia katika kitabu cha kuvunja rekodi ya dunia mwezi Februari mwaka 2022 akiwa na miaka 112 na siku 253.

Juan Vicente Pérez baba wa watoto 11 katika enzi za uhai wake alitumia maisha yake kulima pamoja na kuwa na ustadi wa kusuluhisha migogoro ya ardhi.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post