Aliyeenda ‘baa’ na kutelekeza watoto kwenye gari, awekwa kikaangoni

Aliyeenda ‘baa’ na kutelekeza watoto kwenye gari, awekwa kikaangoni

Mwanamke mmoja kutoka nchini Marekani, aliyetambulika kwa jina la Jamie Leigh Gunn amekamatwa na polisi baada ya kuwaacha watoto wake wawili, moja akiwa umri wa miaka miwili na mwengine miezi nane kwenye gari kisha yeye kwenda ‘baa’.

Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka wa miaka 33 aliwaacha watoto wake kwenye gari kwa zaidi ya dakika 20 peke yao huku gari likiwa halijazimwa na milango ikiwa haijafungwa.

Polisi Jijini Florida wamemkamata na kumfungulia mashitaka ambapo kwa sasa yupo nje kwa dhamana ya Tsh 33 milioni.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post