Agoma kurudi alipotoka, mpaka aonane na Davido

Agoma kurudi alipotoka, mpaka aonane na Davido

Kijana Emmiwuks aliyesafiri siku nane kwa kutumia baiskeli ili aonane na nyota wa muziki kutoka Nigeria, amegoma kurudi kwao baada ya Davido kutoa kauli ya kumtaka kijana huyo arudi alipotoka kwani kwa sasa hayupo Nigeria.

Kutokana na kijana huyo kuweka mgomo wa kurudi kwao kwa kudai kuwa ana zawadi anataka kumpatia Davido, imebidi mkali huyo wa Unavailable amwambie Emmiwuks amtumie ‘akaunti’ namba yake ili ampatie pesa kisha arudi siku nyingine ambayo Davido atakuwepo.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post