Watoto wa chekechea watumia dawa za kulevya

Watoto wa chekechea watumia dawa za kulevya

Dunia ya leo kumekuwa na vitu vingi vya kustaajabisha na kushangaza imekuwa kawaida sana kutokea matukio ambayo huwezi kuya dhania kama yangetokea moja ya tukio lililowapa watu taharuki huko nchini Taiwan.

Watoto wa chekechea kutumia dawa za kulevya shuleni hali ambayo imekuwa na mshanngao na viulizo vingi kisiwani hapo.

Aidha polisi waliweza kugundua swala hilo na kufanya uchunguzi kwa muda wa wiki kadhaa na kusema kuwa haijabainika kwanini watoto hao walikuwa wanapewa dawa za kulevya.

Lakini jambo hilo lilizua balaa kisiwani hapo, baada ya familia za watoto walio athirika kufanya maandamano nje ya majengo ya serikali katika jiji la New Taipei siku ya Jumapili wakitaka uwazi zaidi kutokana na uchunguzi walio ufanya polisi kwa madai kuna vitu havija wekwa wazi.

Chanzo BBC






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post