Wanajeshi 320 Sudan wakimbia kukwepa mapigano

Wanajeshi 320 Sudan wakimbia kukwepa mapigano

Wanajeshi kutoka nchini Sudani wamekimbia nchi yao kukwepa mapigano yanayoendelea na wamekimbilia nchi jirani ya Chad wakihofia kuuawa na wanamgambo wa kikosi cha Rapid Support Forces ‘RSF’ kinachopambana na wanajeshi wa baraza kuu la Sudan lililo chini ya Jenerali Abdel Fattaf al-Burhan

Aidha waziri wa ulinzi wa Chad, Jenerali Daoud Yaya Brahim amesema kuwa "wanajeshi hao waliwasili kwenye ardhi yetu wakipokonywa silaha na kuwekwa kizuizini siku ya Jumapili” alisema Jeneral Daoud

Jeneral huyo aliendelea kuzungumza licha ya vita inayotokea zaidi katika jiji la Khartoum kuwahusu wasudan wao kwa wao lakini wanachukua tahadhari dhidi ya mapigano hiyo ambayo yanadaiwa kusababisha vifo vya watu takribani 270.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post