Vin Diesel atuhumiwa kwa unyanyasaji wa kingono

Vin Diesel atuhumiwa kwa unyanyasaji wa kingono

Muigizaji na producer kutoka nchini #Marekani #VinDiesel anakabiliwa na kesi ya udhalilishaji wa kingono kwa aliyekuwa msaidizi wake aitwaye #Jonasson.

Mkali huyo wa 'Fast & Furious' naye ameingia katika orodha ya ma-star wanaokabiliwa na kesi za unyanyasaji wa kingono baada ya #Jonasson kudai kuwa #Diesel alimlazimisha kufanya naye mapenzi bila makubaliano.

Kufuatiwa na nyaraka za kisheria zilizowasilishwa mahakamani zimeeleza tukio hilo lilitokea mwaka 2010 wakati wa uandaji wa filamu ya ‘Fast 5’ ambapo #Jonasson aliajiriwa na kampuni ya ‘One Race’ kama msaidizi wa #Diesel huku nyaraka hizo zikieleza kuwa tukio hilo lilitokea katika chumba cha muigizaji huyo kwenye hoteli ya ‘St Regis’ jijini #Atlanta.

Aidha mwanadada huyo amedai kuwa alikaa kimya muda wote kwa kuogopa nguvu na ushawishi mkubwa alionao muigizaji huyo.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post