Utafiti: Kukaa kwa muda mrefu kunapunguza siku za kuishi

Utafiti: Kukaa kwa muda mrefu kunapunguza siku za kuishi

Kwa mujibu wa utafiti uliyofanywa na ‘The British Journal of Sports’ umegundua kuwa kukaa chini zaidi ya saa 12 kunaongeza hatari ya kifo cha mapema kwa asilimia 38.

Utafiti huo ulibainika katika Nchi zilizoendelea, ambapo watu wengi hutumia muda mwingi kukaa wakati wa kuendesha shughuli zao za kila siku.

Hata hivyo, imeelezwa kuwa hatari hii inaweza kupunguzwa kwa kufanya mazoezi angalau dakika 22 kila siku.

Aidha utafiti huo ulitoa ushauri kwa watu ambao hawawezi kufanya mazoezi, kwamba wanaweza kujishughulisha katika kazi ndogo zitakazoufanya mwili kuchangamka.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post