Ufahamu mgahawa ambao mteja hujipangia bei ya chakula

Ufahamu mgahawa ambao mteja hujipangia bei ya chakula

Nchini Austria katika mji wa Vienna kuna mgahawa uitwao ‘Der Wiener Deewan’ ambao unatoa ofa kwa walaji wa chakula cha jioni 'diner' kulipa vile ambavyo wao wanaona itakuwa sawa kulingana na walivyokipenda chakula na hali yao ya kiuchumi.

Inaelezwa kuwa ‘Der Wiener Deewan’ ni miongoni mwa migawa inayopendwa katika mji huo ambao ulioanzishwa na wapendanao wawili  Afzaal (Mkimbizi kutoka Pakistani) na Natalie Deewan ambaye ni raia wa Austria.

Kwa mujibu wa Natalie ambaye kwa sasa ni mke wa Afzaal ameeleza kuwa hapo awali walikuwa wamepanga bei ya kuuza, wazo la kuwafanya wateja walipe wanavyojisikia lilikuja mwishoni kwa lengo la kuwasaidia wakimbizi na watu wenye vipato vya nchini nchini humo.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post