Tory atengwa gerezani

Tory atengwa gerezani

Taarifa toka ndani ya gereza alilopo msanii wa Hip-hop Tory zinadai kuwa, mkali huyo wa Hip-hop ametengwa kwenye chumba cha peke yake ambacho ni maalum kwa wafungwa ambao kiusalama hawatakiwi kuchanganywa na wengine gerezani.

Hivyo basi Tory anaruhusiwa kutoka nje ya chumba chake masaa mawili tu kwa siku kwa ajili ya kupunga upepo huku uangalizi dhidi yake unafanyika kila baada ya dakika 30.

Ikumbukwe Tory lanez anashikiliwa gerezani  jijini Los Angeles akisubiri kuhamishiwa gereza jingine kwa ajili ya kuanza kutumikia kifungo chake cha miaka kumi.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post