Sholo Mwamba: Inaniumiza Mama yangu simjui

Sholo Mwamba: Inaniumiza Mama yangu simjui

Mwanamuziki wa nyimbo za #Singeli #SholoMwamba amesema kitu ambacho kinamuumiza kila siku kwenye maisha yake ni kutomfahamu mama yake mzazi.

Amedai kuwa mama yake alifariki wakati yeye akiwa na umri mdogo sana, hiyo basi alipofika umri wa kujitambua alionyeshwa picha ya mama yake tu.

Aidha msanii huyo anaeleza kuwa matamanio yake ni kwamba mama yake angekuwepo kwa wakati huu angefurahi sana.

Sholo hakusita kumshukuru baba yake mazazi kwa malezi aliyo mpatia akishirikiana na mama yake mlezi. Credit XXL






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post