Robertinho aacha walaka kwa Dewji, Kuhusu Azizi Ki

Robertinho aacha walaka kwa Dewji, Kuhusu Azizi Ki

Aliyekuwa ‘Kocha’ Mkuu wa ‘Klabu’ ya Simba Robertinho ameacha walaka kwa Rais wa timu hiyo, Mohammed Dewji na kumtaka amng’oe Aziz Ki Yanga.

Robertinho amekiri kuwa mchezaji huyo ambaye mkataba wake unaelekea ukingoni Yanga ni mashine na kila alipokuwa akikutana naye alikuwa akiweka roho mkononi.

Robertinho amesema kama angeambiwa amchague 'staa' mmoja wa haraka ndani ya kikosi cha mabingwa hao basi angemchagua Aziz Ki pekee na kama kuna bahati kubwa kwa watani wao ni kuwa na mchezaji bora kama raia huyo wa Burkina Faso.

‘Klabu’ ya Simba ilivunja mkataba na Robertinho mapema mwezi huu baada ya kichapo cha bao 5-1 dhidi ya kalbu ya Yanga.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post