Real Madrid yakanusha kumchukua Mbappe

Real Madrid yakanusha kumchukua Mbappe

Baada ya kuibuka kwa tetesi kwamba Real Madrid ilifanya mazungumzo na wawakilishi wa mchezaji wa PSG #KylianMbappe kwa kutaka kumsajili katika dirisha lililopita, ‘mabosi’ wa Madrid waja juu na kukanusha taarifa hizo.

Kupitia taarifa kamili iliyotolewa na ‘timu’ hiyo inaseama kuwa haijafanya mazungumzo na wawakilishi wa mchezaji huyu wala mchezaji mwenyewe.

Mbappe aliingia kwenye sintofahamu na ‘klabu’ yake ya #PSG katika dirisha lililopita, baada ya kudai kuwa ataondoka mwisho wa msimu huu na ‘timu’ hiyo ikatoa uamuzi wa kusaini mkataba mpya na mchezaji huyo au auzwe kwenye ‘klabu’ nyingine na siyo kuondoka bure ‘klabuni’ hapo.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post