Raila Odinga agomea  mualiko wa uapisho wa Ruto

Raila Odinga agomea mualiko wa uapisho wa Ruto

Kutoka huko nchini Kenya wakati shamra shamra za uapisho wa Rais Mteule William Ruto zikiendelea moja kati ya taarifa iliyotufikia Kiongozi wa Azimio La Umoja, Raila Odinga hatahudhuria hafla ya uapisho huo   licha ya kupewa mwaliko binafsi.

Katika taarifa yake siku ya Jumatatu, Odinga alikiri kuwa Ruto alimwalika yeye binafsi kwenye hafla ya kuapishwa lakini akasema hataheshimu mwaliko huo kwa vile yuko nje ya nchi na kwamba bado ana wasiwasi mkubwa kuhusu uchaguzi wa Agosti 9 ambao Ruto alitangazwa mshindi.

Waziri Mkuu huyo wa zamani aliendelea kueleza kuwa mara atakaporejea nchini atatangaza hatua yake nyingine.

Kiongozi huyo amedai kuwa yupo nje ya Nchi, ambapo Odinga amesema anaamini Tume ya Uchaguzi na Mahakama hazikutenda Haki katika Uchaguzi Mkuu wa Agosti 9, 2022 ambao Ruto alitangazwa mshindi.

Hata hivyo ameongeza kuwa, akirejea Kenya atakutana na Viongozi wa Azimio kisha watatangaza hatua watakazochukua ili kuimarisha demokrasia.

"Nikirejea nchini, kwa pamoja na viongozi wa Azimio la Umoja One Kenya Coalition Party, nitatangaza hatua zetu zinazofuata tunapojaribu kuimarisha na kuimarisha demokrasia yetu," alisema.

"Tunaweza tu kufanya hivyo ikiwa tutarekebisha na kubadilisha taasisi muhimu ambazo zina jukumu la kulinda na kuendeleza demokrasia yetu."






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Saphinia Suleiman

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, career, skills development and technology.


Latest Post