Professor Jay: Siyo mchezo kutoka ICU mzima

Professor Jay: Siyo mchezo kutoka ICU mzima

Mwanamuziki mkongwe wa #BongoFleva, #ProfessorJay amedai kuwa kipindi alipokuwa mahututi ICU alishuhudia vifo vya wagonjwa wengi sana.

Akizungumza na chombo cha habari leo asubuhi msanii huyo ameeleza kuwa ingawa magonjwa ni ibada lakini watu wanakufa sana huko ICU tofauti na watu wanavyodhani.

Professor Jay anaeleza kuwa ndani ya siku 127 akiwa ICU ameshudia vifo vya watu wengi na amedai kuwa ukijikuta uko ICU una-survive hata kwa mwezi mmoja siyo mchezo.

Ikumbukwe kuwa taarifa za msanii huyo kuumwa zilianza kusambaa Januari mwaka 2022, na May 4 mwaka huu aliweza kuonekana tena akiwa mzima na kuendelea na majukumu yake kama awali.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post