Priske achukua mikoba ya Slot

Priske achukua mikoba ya Slot

Klabu ya Feyenoord kutoka Uholanzi imemteua Brian Priske kuwa kocha mkuu katika kikosi hicho akichukua mikoba ya Arne Slot aliyetimkia klabu ya #Liverpool.

Priske mwenye umri wa miaka 47 raia wa Denmark ambaye amewahi kuinoa klabu ya Royal Antwerp ya Ubelgiji hivi karibuni alikuwa akiifundisha ‘timu’ ya Sparta Praha ambayo ameiongoza kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Jamhuri ya Czech mara mbili mfululizo.

Hata hivyo Priske mwaka 2019 hadi 2021 aliwahi kuifundisha klabu ya #FCMidtjylland, ambapo alisimamia michezo 68 na kukusanya alama 188 na kuondoka na taji la ligi mwaka 2019 na 2020.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post