Petit amkataa Mourinho

Petit amkataa Mourinho

Baada ya kuzuka tetesi kuhusiana na ‘klabu’ ya #Chelsea kutaka kumsajili ‘kocha’ #JoseMourinho, mchezaji wa zamani wa Chelsea na Arsenal #EmmanuelPetit ametoa ushauri kwa ‘timu’ hiyo kwa kudai kuwa uwamuzi huo siyo sahihi

Kwa mujibu wa The Sun News inaelezwa kuwa Petit ambaye aliwahi kuichezea ‘klabu’ hiyo kutoka mwaka 2001 hadi 2004 anaamini  kuwa #Chelsea inahitaji ‘kocha’ atakaeirudisha ‘timu’ hiyo katika ubora wake.

Mbali ya kumkataa #Mourinho, #Petit ametaja baadhi ya ma-kocha ambao anaona wanweza kuwa chaguo sahihi kwa ‘klabu’ hiyo akiwemo ‘kocha’ wa #Arsenal #MikelArteta.

Wazo la kusaka ‘kocha’ mpya ‘klabuni’ hapo linakuja baada ya mashabiki kumkataa ‘kocha’ mkuu #MauricioPochettino kutokana na matokeao mabovu anayoyapata.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post