Osimhen afichua kinachofanya avae Maski

Osimhen afichua kinachofanya avae Maski

Nyota wa Napoli na mchezaji wa kimataifa kutoka nchini Nigeria, Victor Osimhen amefichua sababu za kutumia maski ya kuficha sehemu ya macho katika kila ‘mechi’.

Kupitia mahojiano yake ya hivi karibu na Brilla FM, ameweka wazi kuwa huvaa maski hiyo kwa ajili ya kujikinga kwani bado ana 'skrubu' mbili kwenye taya na uso hivyo zinamlazimu kuvaa 'maski' hiyo maisha yake yote ya ‘soka’.

Osimhen alifanyiwa upasuaji wa uso baada ya kugongana na ‘beki’ wa Inter Milan Skriniar katika mechi iliyochezwa Oktoba mwaka 2021.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post