Nini kimetokea kati ya Niffer na Alikiba

Nini kimetokea kati ya Niffer na Alikiba

Baada ya kuwa na ‘skendo’ za kimapenzi kati ya mwanadada Niffer na AliKiba, wawili hao bado wameendelea kuwaacha watu katika maswali yasiyo na majibu, baada ya mrembo huyo kufuta picha za King huku akishusha ujumbe mzito kwenye ukurasa wake wa Snapchat3.

Awali mwanadada huyo aliweka picha ya #King kwenye profile picture yake ya Instagram, lakini cha kushangaza ni kwamba hivi sasa picha hiyo haipo tena katika ukurasa huo, si hivyo tu bali Niffer amefuta urafiki na #Kiba katika mtandao wa #Instagram.

Ujumbe wa Niffer umepelekea watu kuhusianisha tukio hilo na kile alicho kiandika huku wengi wakidai kuwa huenda wawili hao wameachana na ndio maana Niffer kamu-unfollow King kwenye Instagram.

Kupitia #Snapchat ya Niffer ameandika ujumbe usomekao

“Unachoweza kufanya nikujua mtu atakae jua thamani yako, jipe nafasi yako zaidi using’ang’anie mtu ambae hakutaki na kisha kukuonyesha kila aina ya vituko”






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post