‘Rapa’ kutoka nchini #Marekani Nick Minaj amefikiria kujumuisha nchi ya #Nigeria katika ziara yake ikiwa tuu mashabiki wa nchi hiyo watajisajiri na kununua ‘tiketi’ za kutosha.
Mmoja wa shabiki nchini humo ‘ali-tweet’ kwenye moja ya post ya #Nick kwa kuweka wazi kuwa Afrika imetengwa katika ziara kubwa kama hizo ambapo #Nick aliweka wazi kuwa endapo mashabiki hao wako serious basi wajisajili kwa ajili ya kununua ‘tiketi’ huku akidai kuwa nchi hiyo huenda ikawa ya mwisho kwenye tour yake.
#Tour hiyo aliyoipa jina la ‘Pink Friday 2 Tour' inayotaraija kufanyika mwaka 2024 ambapo kwa sasa bado ‘tiketi’ hazijatolewa lakini mashabiki wanaweza kujisajili ili tiketi zitakapotoka wawe wa kwanza kupata.

Leave a Reply