Naira Marley na Sam wapambana kurudisha heshima yao

Naira Marley na Sam wapambana kurudisha heshima yao

Mwanamuziki kutoka nchini #Nigeria #NairaMarley, na promota #SamLarry baada ya jana kuonekana kwa mara ya kwanza tangu kuachiwa kwao, waawili hao waliamua kutoa sadaka kwa watu wenye uhitaji huku baadhi ya wadau wa muziki nchini humo wakidai kuwa wawili hao huenda wanataka kurudisha Imani yao katika jamii.

#Naira, #Sam na #Zinoleesky walikwenda katika nyumba ya watoto yatima huko #Lagos na kugawa chakula pamoja na mahitaji mengine jambao ambalo lilizua gumzo mitandaoni huku watu wakiwataka wawili hao kuacha kubadilisha mawazo ya watu kwasababu wanajua walicho kifanya na hawato weza kusahau tukio hilo.

Hii ni mara ya kwanza wawili hao kuonekana wakiwa pamoja tangu kutokea kifo cha mwanamuziki #Mohbad kilichotokea Septemba 12 mwaka huu.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post