Naira amgeuzia kibao muigizaji iyabo kisa kifo cha Mohbad

Naira amgeuzia kibao muigizaji iyabo kisa kifo cha Mohbad

Mwanamuziki kutoka nchini Nigeria #NairaMarley ametishia kumshtaki muigizaji kutoka nchini humo #IyaboOjo kwa madai ya kumchafua kwa kuchapisha habari za uongo kipindi akikabiliwa na tuhuma za mauaji ya aliyekuwa #Mohbad.

#Naira ameweka wazi kuwa atamshtaki muigizaji huyo kwa fidia ya dola 632,807 ambazo ni zaidi ya tsh 1.5 bilioni, iwapo hatomuomba msamaha kwa alichokifanya. #NairaMarley akiwakilishwa na wakili wake #OlalekanOjo(SAN) na Co, amemuandikia barua #Iyabo barua, akimshutumu kwa kuchapisha maudhui ya uongo kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Aidha wakili huyo anayemwakilisha #NairaMarley ameomba muigizaji huyo aombe msamaha kwenye akaunti yake ya Instagram na katika gazeti la kitaifa kila siku ndani ya siku 7 baada ya kupokea barua hiyo kabla hawajachukua hatua za kisheria.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post