Mwijaku kufungua radio Kazuramimba

Mwijaku kufungua radio Kazuramimba

Wakati baadhi ya wamiliki wa media nchini  wakiendelea kuboresha vituo vyao vya habari ili kupata wafuatiliaji zaidi, hatimaye mtangazaji na mwanamitandao Mwijaku amedai kuwa anatarajia kufungua radio yake mkoani Kigoma.

Mwijaku ameyasema hayo kupitia ukurasa wake wa X kwa kueleza kuwa anawaza kufungua radio Kigoma na anaona ni wakati wake sahihi wa kuisimamisha Kazuramimba kwenye ramani, na kueleza kuwa atapita kwa wawekezaji kuwapa dokezo huku akihitaji  tsh 1.5 bilioni  ili kuwezesha kufungua radio hiyo  aliyoipa jina la Mwijaku FM.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post