Mume amuacha mkewe kwa kumuita mama mkwe mchawi

Mume amuacha mkewe kwa kumuita mama mkwe mchawi

Mwanamume moja alifahamika kwa kwa jina la Agyei Mensa raia wa Ghana anaeishi nchini Sweden alikatisha ndoa yake na mke wake mpendwa hali hambayo imezua taharuki katika mitandao ya kijamii  mwanamume huyo anayeishi nje ya nchi alieleza kuwa mke wake wa zamani hakuwa na heshima.

Hali ambayo ilipelekea kufanya mipango ya kuhakikisha kwamba watoto wake wanapata mafunzo yanayofaa ya nyumbani nchini Ghana na sio Sweden anakoishi.

Mwamba huyo alisema tabia ya mkewe ya kukosa heshima ilisababisha ndoa yao kuvunjika akizungumza katika mahojiano yalio fanyika katika chombo kimoja cha habari Afrika  na kwenye mitandao alisema sababu kubwa iliyomfanya aondoke kwenye ndoa yake ya awali ni kutokana na tabia mbaya ya mkewe kuwadharau ndugu zake.

Akieleza kwa kina jamaa huyo alisema sifa moja ambayo hakuipenda kwa mke wake ni jinsi alivyowadharau ndugu na marafiki na kuvuka mipaka hadi kwa mama yake mzazi, kwa kumtamkia kuwa mchawi ndipo akachukua jukumu la kumuacha mkewe huyo.

Chanzo Tuko






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post