Mtoto wa Mugabe ataka kulipwa million 6 kwa ajili ya child support

Mtoto wa Mugabe ataka kulipwa million 6 kwa ajili ya child support

Mtoto wa Kike wa Aliekuwa Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe, Bona Ouma Mugabe katika madai ya talaka ametaka kupatiwa hela ya matumizi ya watoto Milioni 6.3 kwa watoto watatu kila Mwezi.

Bona na mume wake Simbarashe Mutsahuni walifunga ndoa ya kifahari mnamo mwaka 2014 harusi hiyo, inayokadiriwa kugharimu dola milioni 4 (zaidi ya Biloni 9.4 za kitanzania) na ilionyeshwa moja kwa moja (live) kwenye runinga ya serikali.

Siku ya harusi baba wa Bona  aliwazawadia kiasi cha Pesa Tsh.Milioni 235 na Ng'ombe 55, binti huyo aliwasilisha dai hilo la talaka mapema March, 2023 huku akisema kuwa wamekuwa na tofauti ndani ya nyumba kwa Miezi 9.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post