Mlinzi anayetuhumiwa kufanya mapenzi na maiti akamatwa

Mlinzi anayetuhumiwa kufanya mapenzi na maiti akamatwa

Mwanaume mmoja kutoka nchini Marekani aitwaye Randall Bird ambaye ni mlinzi katika chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali ya Phoenix, KPHO aliyetuhumiwa kufanya mapenzi na maiti akamatwa.

Tukio hilo lilitokea Oktoba 22, kesi yake ilisikilizwa Jumanne ya wiki aliyoisha ambapo Brid alifunguliwa mashitaka matano moja wapo likiwa la kumfanyia uhalifu na mtu aliyefariki.

Aidha mashuhuda wawili walisimamishwa kizimbani na kueleza kuwa walimuacha Bwana Brid alinde wakati wao walipokwenda kupata chakula cha usiku mara tuu baada ya kurudi walikuta mlango wa chumba hicho cha kuhifadhia maiti ulikuwa umefungwa kwa ndani.

Huku wakidai kuwa mtuhumiwa huyo alitoka nje akiwa hajafunga zipu na mkanda wa suruali yake na kuonekana akiwa anatokwa jasho.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post