Mke wa Kanye amefikia pabaya

Mke wa Kanye amefikia pabaya

Kama ilivyo kawaida kwa wanandoa hawa #KanyeWest na #BiancaCensori kuvaa mavazi ya kushangaza katika jamii, hivi karibuni mke wa Kanye amezua taharuki kwa watu nchini  Italy baada ya kuvaa vazi lenye kuonesha utupu wake.

Bianca alionekana akiwa katika vazi ambalo limetafsiriwa kama ukosefu wa maadili kwenye jamii ambalo limekuwa  likimuonesha mtupu huku akikatiza mitaani.

Kwa mujibu wa tovuti ya TMZ imeripoti kuwa, raia wa maeneo aliyopita Bianca walishangazwa na uvaaji huo na kushindwa kuvumilia hadi kutoa taarifa polisi kwa kuripoti juu ya vitendo hivyo ambavyo kwa mujibu wa sheria za Italy hupelekea kutozwa faini ya zaidi ya TSh 25 milioni au kifungo cha miaka 4.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post