Mayweather amkumbuka msaidizi wake

Mayweather amkumbuka msaidizi wake

Bondia wa zamani na promoter kutoka nchini Marekani #LoydMayweather ameangua kilio baada ya kumkumbuka msaidizi wake wa kazi za nyumbani aliyefariki mwaka jana akiwa na umri wa miaka 47.

Kupitia mahojiano yake na #Pivot Mayweather ameeleza kuwa msaidizi wake aliyejulikana kwa jina la Marikit Laurico alikuwa kama rafiki yake kwa sababu alikuwa anajua siri zake nyingi.

Marikit Laurico alifariki mwaka jana baada ya kusumbuliwa na matatizo ya Kiafya kwa muda mrefu, na alifanya kazi nyumbani kwa bondia huyo kwa miaka 25.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post