Marioo atoa onyo kwa wanaomsumbua Paula

Marioo atoa onyo kwa wanaomsumbua Paula

Mwanamuziki wa #BongoFleva, nchini #Marioo ametoa onyo kwa ‘mastaa’ wakiume wanaomsumbua mpenzi wake #PaulaKajala katika mitandao ya kijamii hususani #Instagram.

Marioo ametoa onyo hilo kupitia mahojiano yake na moja ya chombo cha habari nchini akiweka wazi kuwa anawajua wote wanaomsumbua mpenzi wake kwa kumtumia jumbe za kumtaka kimapenzi.

Hivyo basi amewataka watu hao kuacha mara moja huku akitilia mkazo kuwa endapo wataendelea basi hatosita kuwafichua hata wakiwa watu wake wa karibu.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post