JOSLIN: Barnaba anitafute tuyajenge

JOSLIN: Barnaba anitafute tuyajenge

Msanii wa miundo ya RnB, Joslin amemtaka msanii wa kizazi kipya Barnaba kumtafuta ili kuongelea suala la msanii huyo tuimba nyimbo yake ya "Niite Basi" kwenye majukwaa mbalimbali ya muziki.

Kupitia kipindi cha Big Sunday Live, Joslin amesema kuwa amesikia Barnaba akiimba nyimbo yake, hakuichukulia vibaya ila aliandika ujumbe kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram kuomba waonane na kuongea, kitendo kilichopokelewa tofauti zaidi na mashabiki.

"Siku sema hivyo kwa ubaya, wengi waliichukulia serious," aliongeza msanii huyo.

"Sio mara ya kwanza kuona hivyo" alisema Joslin.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Detricia Pamba

A Digital Journalist, Content Creation Executive at Mwananchi Communications Ltd and Chief Editor of Mwananchi Scoop. I'm also writes stories around Technology, every Wednesday on Mwananchi Scoop. My other famous segments on Mwananchi Scoop include LISTI and WHO’S HOT.


Latest Post