J.Cole afuta ngoma ya 7 minute Drill

J.Cole afuta ngoma ya 7 minute Drill

Baada ya mwanamuziki kutoka nchini Marekani J.Cole kumuomba msamaha Kendrick Lamara katika onesho la Dream Ville lililofanyika wiki hii, kuhusiana na kumsema vibaya Lamar kupitia wimbo wake mpya wa ‘7Minute Drill’ sasa imeripotiwa kuwa Cole amefuta ngoma hiyo katika majukwaa yote ya kuskiliza muziki.

Kupitia wimbo huo mpya Cole alimchana Kendrick kuwa amepotea kwenye game ila baada ya kutoa wimbo wake wa ‘Diss’ ndiyo mashabiki wameanza kumfuatilia.

Ikumbukwe pia wawili hao wamewahi kufanya ngoma za pamoja kama ‘Black Frida, ‘Like That’, ‘temptation’, ‘The Millennials Folklore’ na ‘Forbidden Fruit’.

Ngoma hiyo ya ‘7Minute Drill’ ipo katika albumu yake mpya iitwayo ‘Might Delete Later’ iliyotoka Jumamosi, ya April 6,






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post