Idadi ya wanaochukia tattoo walizochora yaongezeka

Idadi ya wanaochukia tattoo walizochora yaongezeka

Kulingana na uchunguzi wa kitaifa uliyofanywa na ‘Advanced Dermatology’ kutoka Illinois, Marekani umebaini kuwa idadi ya wanaochukia tattoo walizochora yaongezeka.

Katika uchunguzi huo uliyofanywa kwa kipindi cha mwaka mmoja ulibaini kuwa idadi ya waliotaka kufuta tattoo zao imefikia asilimia 51 ikiipiku idadi ya awali ikiwa asilimia 15.

Aidha Dk. Alissa Lamoureaux, daktari wa ngozi aliyeidhinishwa na bodi huko Shrewsbury, alieleza kuwa watu hutaka kuondolewa tattoo zao kutokana na umri wao kwenda.

“Ni watu wa umri kuanzai 30-40, huwenda walichora tattoo hizo wakiwa wadogo na sasa wanaona ni kama fashioni hiyo imepitwa na wakati katika umri wao” amesema.

Vipi bado unamapenzi na tattoo yako, au nawewe unataka kuifuta?






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post