Idadi ya mamilionea yaongezeka

Idadi ya mamilionea yaongezeka

Idadi ya mamilionea kutoka katika jiji la New York nchini Marekani imeongezeka katika miaka ya hivi karibuni huku ikikadiriwa kuwa mmoja kati ya wakazi 24 anatajwa kuwa ni milionea.

Kwa mujibu wa ‘Global Ranking’ imeeleza kuwa mpaka kufikia sasa jiji hilo lina zaidi ya mamilionea 350,000 ikifikia asilimia 48 kutoka 36 kati ya mwaka 2013 hadi 2023.

Hata hivyo kulingana na kampuni ya ushauri wa uhamiaji ya ‘Henley & Partners’ imebaini kuwa watu hao 350, 000 wana utajiri wa fedha taslimu kiasi cha dola 1 milioni ikiwa ni sawa na Sh 2.5 bilioni.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post