H Money adondosha Tic Tik na Reekado Banks

H Money adondosha Tic Tik na Reekado Banks

Prodyuza wa muziki wa kimataifa, Harmony Samuels a.k.a H Money, ameachia wimbo mpya uitwao 'Tic Tik' akimshirikisha gwiji kutoka Nigeria, Reekado Banks.

Katika wimbo huo wenye mikito ya Kinigeria, ladha tamu kutoka kwa H-Money akiungana na Reekado, unatengeneza burudani ya aina yake ya mtindo wa Afrobeats uliotayarishwa kwa umaridadi wa juu.

Tic Tik inaashiria mwanzo mpya wa muziki kwa H-Money aliyewahi kufanya kazi na wasanii kama Ariana Grande, Jennifer Lopez, Maroon 5, Rick Ross, Fifth Harmony, Mary J. Blige na wengineo. Akizungumzia wimbo huo, H-Money anasema: "Tic Tik ni wimbo wangu wa kwanza katika mwanzo mpya wa muziki wa AfroBeats ukiwa na mchanganyiko wa R&B, unaozingatia tamaduni zetu, huku ukiwashirikisha wasanii wakali.”

Wimbo huo sio tu unaonyesha ushirikiano wa kusisimua kati ya wasanii wawili wenye nguvu kubwa katika muziki, lakini unatumika kama hatua muhimu katika safari ya kisanii ya H-Money anapojitosa katika ulimwengu mahiri wa Afrobeats.






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post