Dorah atoa povu wanaosema hawezi kuwa na mahusiano

Dorah atoa povu wanaosema hawezi kuwa na mahusiano

Muigizaji wa #BongoMovie, ambaye alijulikana zaidi kupitia tamthilia ya ‘Jua Kali’  #Dorah ameeleza kuwa anachukizwa na watu wanaosema kuwa hawezi kuwa na Mahusiano kwa sababu ya kuonewa huruma jinsi alivyo.

Dorah ameyasema hayo akiwa katika mahojiano na mmoja ya chombo cha habari ambapo ameeleza hisia zake na kuwaonya watu wanaoendelea kumsema hawezi kuwa na mpenzi huku akiwataka waache mara moja kwani hajiskiii vizuri kuona baadhi ya watu kumuona ni mtu wa tofauti na wengine.

Hata hivyo ameweka wazi kuwa yeye anampenzi na mahusiano yake ni ya muda mrefu lakini hawezi kum-post mpenzi wake katika mindao ya kijamii kwa sababu ni maisha yake private hivyo haina haja kila mtu kuyajua.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post