Davido kama Drake

Davido kama Drake

Mkali wa Afrobeat kutoka nchini Nigeria Davido ameamua kufuata nyayo za ‘rapa’ Drake baada ya kumlipia mwanafunzi mkopo wa shule.

Mwanafunzi huyo alinyanyua bango kwenye show ya Davido iliyofanyika katika ukumbi wa ‘Madison Square Garden’ likieleza kuwa anaomba msaada wa kulipiwa mkopo wa shule, ndipo msanii hiyo akaeleza kuwa atamchangia dola 50k sawa na Sh 129 milioni.

Matukio kama haya yamekuwa ya kawaida kwa mwanamuziki Drake, kwani miezi kadhaa iliyopita amekuwa akitoa maokoto kwa mashabiki wake moja wapo ikiwa ya kumlipia shabiki mkopo wa nyumba uliyokuwa ukigharimu kiasi cha dola 160k ambayo ni sawa na Sh 408 milioni.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post