CAF waomba radhi baada ya Berkane kususia mechi

CAF waomba radhi baada ya Berkane kususia mechi

Shirikisho la Soka Afrika (CAF) limeomba radhi wadau wa soka baada ya mechi ya kwanza ya nusu fainali ya mashindano ya kombe la shirikisho kutofanyika baada ya ‘klabu’ ya RS Berkane kugoma kucheza jana Jumapili.

‘Timu’ hiyo kutoka nchini Morocco iliamua kuondoka uwanjani muda mfupi kabla ya mechi hiyo dhidi ya UsmAlger, baada ya mamlaka nchini Algeria kuizuia kutumia ‘jezi’ zao zenye ramani ya Morocco inayojumuisha eneo lenye mgogoro wa kisiasa.

Awali CAF iliagiza mamlaka nchini Algeria iwarejeshee RS Berkane ‘jezi’ hizo, lakini ‘timu’ ilipofika vyumba vya kubadilishia nguo haikuzikuta na ndipo ikaamua kugeuza na kuondoka uwanjani.

Katika taarifa iliyowekwa kwenye tovuti ya CAF imesema suala hilo litapelekwa kwenye chombo kinachohusika kwa ajili ya uamuzi na kuomba radhi kwa mashabiki.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post