Baada ya mika sita ya uchumba Eddie Murphy afunga ndoa

Baada ya mika sita ya uchumba Eddie Murphy afunga ndoa

Mwigizaji kutoka nchini Marekani, Eddie Murphy amefunga ndoa na mpenzi wake wa Paige Butcher baada ya kudumu mika sita kwenye uchumba.

Inaelezwa kuwa wanandoa hao waliokuwa kwenye uchumba kwa takriban miaka miaka sita, walifunga ndoa katika sherehe ya faragha iliyojumuisha familia na marafiki wachache wa karibu.

Hata hivyo harusi ya wawili hao ilfanyika Julai 9, akitka kijiji cha Anguilla kwenye visiwa vya Caribbean.

Eddie Murphy mwenye umri wa miaka  66 na mke wake mwanamitindo wa kutoka nchini Australia, Paige Butcher, mwenye umri wa miaka 44 waliingia kwenye uchumba mwaka 2018.

Mwigizaji huyo amewahi kufanya filamu kama, Trading Place, Tower Heist, Boomerang, Coming 2 America, Beverly Hills Cop III, Norbit na nyingine nyingi.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post