Aliyekuwa mke wa Mohabad agoma kutoa dna ya mtoto

Aliyekuwa mke wa Mohabad agoma kutoa dna ya mtoto

Aliyekuwa mke wa marehemu #Mohbad, amegoma mtoto wake kupimwa DNA baada ya watu kumshutumu kuwa huwenda mtoto huyo sio wa marehemu Mohbad.

Kwa mujibu wa Gossiptv News imeeleza kuwa mwanadada huyo amesema kuwa hataweza kutoa DNA ya mwanaye na hakuna anayeweza kumuamrisha kufanya hivyo, huku akidai hakuwahi kuwa na mwanaume mwengine alipokuwa na marehemu mume wake.

Mohbad alifariki Septemba 12 mwaka jana katika mazingira ya kutatanisha hali ambayo ilipelekea baadhi ya ‘mastaa’ kukamatwa kwa kuhusishwa na kifo hicho akiwemo Naira Marley pamoja na Sam Larry. ambao kwasasa wapo uraiani baada ya kuachiwa kwa dhamana.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post