Album ya Tyla yazidi kukimbiza Billboard

Album ya Tyla yazidi kukimbiza Billboard

Album ya mwanamuziki kutoka Afrika Kusini Tyla iitwayo ‘TYLA’ kwa mara ya kwanza imeshika namba moja kwenye chart za ‘Billboard World Album Chart’, huku ikiwa album yake ya kwanza kushika namba moja katika chart hizo.

Hii inakuwa album ya pili kwa mwanamuziki wa Africa kushika namba moja Billboard ya kwanza ikiwa ya Wizkid iitwayo ‘Made in Logos’.

Albumu hiyo yenye ngoma 14 iliachiwa rasmi Machi 22, mwaka huu huku baadhi ya ma-staa kutoka Marekani wakishilikishwa akiwemo #TravisScott, #KelvinMomo na wengineo.

.

.

#MwananchiScoop

#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post