Aiumbua Benki kwa kumpa pesa bandia

Aiumbua Benki kwa kumpa pesa bandia

Mwanaume mmoja kutoka nchini #Nigeria aliyefahamika kwa jina la #LegendaryPapi ameiumbua ‘benki’ iliyoko nchini humo baada ya kumpa pesa bandia kiasi cha Euro 5000 ambazo ni zaidi ya million 13 za Kitanzania.

Kwa mujibu wa #Battaboc news imeeleza kuwa kupitia ukurasa wa #X wa mteja huyo aliweka wazi kuwa alitoa pesa kwenye tawi la benki kwa lengo la kumpa rafiki yake aliyekuwa akisafiri kwenda #Uingereza ambapo pesa hizo ziligundulika kuwa bandia baada ya rafiki yake huyo kwenda kubadilisha pesa hizo kuwa #Pounds.

#Papi aliweka wazi suala hilo kutokana na ‘benki’ hiyo kutomrudishia pesa zake ambazo amezitafuta kwa jasho.
.
.
#mwananchiscoop
#burudikanasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post