AFL sheria ya bao la ugenini ipo palepale

AFL sheria ya bao la ugenini ipo palepale

Kwa mujibu wa kanuni za mashindano ya African Football league (AFL) kuelekea mchezo wa kesho kati ya Al Ahly dhidi ya Simba lile bao la ugenini lipo.

Kanuni ya 15 kifungu kidogo cha tatu kimeondoa sintofahamu hiyo ikiweka wazi kwamba kwa ‘mechi’ za hatua ya robo fainali, nusu fainali ‘timu’ itakayokuwa na idadi kubwa ya mabao ya ugenini itafuzu hatua inayofuata.

Kanuni hiyo hiyo kipengele kinachofuata ikaeleza kuwa bao hilo la ugenini linatumika mpaka kwenye mchezo wa fainali ambapo timu yenye mabao mengi baada ya mechi ya pili itachukua ubingwa.

Kwa upande wa kanuni ya 16 kipengele cha kwanza nacho kimeeleza kuwa kuanzia hatua ya robo fainali endapo timu zote zitalingana kwa mabao ya kufunga na yale ya ugenini ‘mechi’ hiyo itaamuliwa kwa mikwaju ya ‘penati’.

Ufafanuzi huo unaifanya Simba kesho kuendelea kuupigania ushindi kwenye mchezo huo wa ugenini au sare ya mabao 3-3 na zaidi ili iweze kutinga hatua ya nusu ‘fainali’.

Simba ilipata ‘sare’ ya mabao 2-2 hapa nyumbani Uwanja wa Benjamin Mkapa dhidi ya Ahly ambao ni mabingwa wa Afrika na kesho saa 11 jioni ‘timu’ hizo zitamalizana kwa mchezo wa pili wamarudiano utakaopigwa Jijini Cairo nchini Misri.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Asha Charles


Latest Post