Adidas kuuza mzigo wote wa Kanye

Adidas kuuza mzigo wote wa Kanye

Kampuni inayojihusisha na utengenezaji wa vifaa vya michezo na mavazi ya Adidas kutoka nchini Ujerumani imetanganza kuuza bidhaa zote za Kanye West zilizopo ndani (stock).

Hii inakuja baada ya mapato kushuka katika kampuni hiyo tofauti na kiwango walichokuwa wakikiingiza mwaka 2022. Aidha mwaka jana Adidas ilitangaza inatarajia kupata hasara ya dola 1.3 bilioni iwapo hawatouza mzigo wote wa Kanye uliopo ndani (stock).

Adidas ilivunja mkataba na ‘rapa’ Kanye Oktoba 2022 kufuatiwa na kauli ya Kanye ya chuki dhidi ya Wayahudi.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post